Monday 12 December 2011

tanzania ikiwainaendelea kusherekea miaka yake 50 ya uhuru wengine waendelea kulia machozi

wakati tanzania ikiendelea kujivunia maadhimisho yake ya miaka 50 ya uhuru kwa upande mwingine wananchi wameendelea ku bubujika machozi makundi hayo ni pamoja na ma albino ambao wamekiri kuwa miaka hiyo kwao ni kama kusherekea kunyanyaswa na kutengwa kwaajili ya ulemavu wao, kundi lingine ni maskini ambao wanachukua nafasi kubwa sana katika nchi hii, kwani imeonekana dhahili kuwa maskini ataendelea kuitwa maskini hadi kifo chake na tajiri kuwa tajiri zaidi. tovuti yetu ilifanya mkakati wa kumtafuta kiongozi yeyote mwenye wadhifa katika serikali yetu kwaajili ya kufahamu kero hii itakwisha lini ya kuweka usawa na kupunguza gepu la tabaka lililopo kati ya maskini na tajiri lakini viongozi walio wengi hawakuweza kuwa na muda wa kulijibu swali hilo. ukweli ni kwamba iko haja ya serikali yetu kuangalia swala hilo na kuwapunguzia makali ya maisha wananchi hasa wale wa kipato cha chini

No comments:

Post a Comment