Tuesday 13 December 2011

MVUA KUBWA ILIYONYESHA ENEO KUBWA YA JIJI LA DAR ES SALAAM YAUWA MMOJA ENEO LA MZAMBARAUNI SHULENI

Siku ya jana majira ya asubuhi baada ya mvua kubwa iliyonyesha maeneo mengi ya jiji hili likiwemo eneo moja lijulikanalo kama shule ya msingi mzambarauni lililopo wilaya ya ilala kata ya ukonga, limetokea tukio moja la kusikitisha na kuuzunisha kwani kipindi mvua hiyo inaendelea kulikuwepo na watu watano waliokuwa chini ya mti wa mwembe wakijisitiri mvua isiweze kuwalowanisha pia miongoni mwao wakisubiri usafiri, ndipo baada ya muda mfupi ulitokea upeepo mkali uliopelekea kuangusha mwembe huo ambao ukaangukia mbuyu hivyo kupelekea kuanguka kwa mwembe pamoja na mbuyu. wote walifanikiwa kuuona pindi unaanza kukatika ndipo watu wanne wakafanikiwa kuukimbia na kukwepa kabla haujaanguka lakini dada mmoja alishindwa hivyo kupeelekea mwembe huo kumwangukia na kupoteza maisha papo hapo, baada ya dakika chache wasamalia wema walifanikiwa kuutoa mwili wa marehemu na kuukimbiza hospital. uchunguzi wa awali ulionyesha marehemu ni mkazi wa eneo hilo la mzambarauni MWENYEZI MUNGU aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi amen. hadi siku ya leo mkakati unaendelea wa kuukata na kuuondoa kabisa mwembe na mbuyu eneo hilo la tukio.

No comments:

Post a Comment