Tuesday 9 August 2011

moja ya nyumba iliyochomwa moto katika fujo mjini london


ePolisi  wa  Uingereza  wakiwa  wamesimama  karibu  na  jengo  lililochomwa  moto mashariki  ya  London

Moto umeendelea kuwaka mjini London kwa siku ya tatu mfululizo wakati ghasia na hali isiyo tulivu vikiongezeka. Waziri mkuu David Cameron amekatiza mapumziko yake nchini Italia.

 
Moto  unaendelea  kuwaka  mjini  London  kwa  siku  ya  tatu mfululizo  wakati  ghasia  na  hali  isiyo  tulivu  vikiongezeka. Waziri mkuu  David Cameron  amekatisha  mapumziko  yake  nchini  Italia na  kurejea   mjini  humo  na  anatarajiwa  kukutana  na  kamati  ya ngazi  ya  juu  ya  kushughulikia  masuala  ya  dharura    leo Jumanne. Wakati  huo  huo , ghasia  hizo , ikiwa  ni  pamoja  na uporaji  ,uchomaji  magari  na  majengo , umesambaa  katika maeneo  mapya  mjini  London  na  katika  miji  ya  Birmingham  na Liverpool. Ghasia  hizo  zilianzia  Tottenham  siku  ya  Jumamosi baada  ya  maandamano  dhidi  ya  polisi  kugeuka kuwa  ghasia. Hata  hivyo  waziri  wa  mambo  ya  ndani  Theresa May ameshutumu  ghasia  hizo  kuwa  ni  uhalifu.Waziri  mkuu David Cameron  amekatiza  mapumziko  yake  nchini  Italia  na  kurejea  mjini  London.Waziri mkuu David Cameron amekatiza mapumziko yake nchini Italia na kurejea mjini London.

No comments:

Post a Comment