Tuesday 30 August 2011

Majeshi ya Gaddafi yatakiwa kusalimu amri



Libya
Viongozi wa waasi wa Libya wamewapa majeshi yanayomwuunga mkono Kanali Gaddafi mpaka Jumamosi kusalimu amri au kukabiliana na majeshi.
Mustafa Abdul Jalil, anayeongoza Baraza la Mpito la Taifa (NTC), alisema onyo hilo limeelekezwa kwa wanaomtii Kanali Muammar Gaddafi waliopo mji alipozaliwa wa Sirte na katika miji mengine.
Tangazo hilo limetolewa baada ya mke wa Kanali Gaddafi na watoto wake watatu kukimbilia nchi jirani ya Algeria.
Algeria imejitetea kwa hatua hiyo waliochukua, huku waasi wakiita " kitendo cha kiburi".
Mpaka sasa mahala alipo Kanali Gaddafi haijulikani.
Wakati huo huo huo huko Libya, waasi wanajaribu kupambana na wanaomtii Gaddafi, na kujiandaa kusogea Sirte.

No comments:

Post a Comment